Kamati ya Nidhamu ya Simba yamuhoji Aussems kwa takriban saa moja!
Kamati ya Nidhamu ya klabu ya Simba jana Alhamis Novemba 28, 2019 imemuhoji kocha Mkuu wa timu hiyo Patrick Aussems ambaye anakabiliwa na tuhuma mbalimbali
Kamati hiyo iliyoongozwa na Mwanasheria Michael Muhina, ilikutana na Aussems katika kikao kilichoanza saa 11 jioni mpaka saa 12 na nusu
Uongozi wa Simba bado haujaweka wazi kuhusu maazimio yaliyofikiwa kwenye kikao hicho huenda hapo kesho Mtendaji Mkuu Senzo Mazingisa atazungumza
Kitambi aendelea kusimamia mazoezi
Wakati hatma ya Aussems ikisubiri uamuzi baada ya kikao hicho, kocha msaidizi Denis Kitambi leo ameongoza mazoezi ya kikosi cha Simba kwa siku ya tatu
Kitambi amesema leo wachezaji wameonyesha kuchangamka tofauti na hali ilivyokuwa siku mbili zilizopita
Hata hivyo amesema kukosekana kwa kocha Aussems mazoezini kunawaweka wachezaji katika wakati mgumu.
Post a Comment