Ads

KAMPUNI YA RELI TANZANIA(TRL)




Taarifa kwa Vyombo vya Habari (Press release)


HATIMAYE ABIRIA 540  WA TRENI YA DELUXE WALIOKWAMA STESHENI YA SOGA MKOANI PWANI  WAMESAFIRISHWA KWA MABASI 9 KUJA DAR ES SALAAM LEO JUMATATU NOVEMBA 28, 2016



Abiria 540 wa treni ya Deluxe iliokwama katika stesheni ya Soga mkoani Pwani jana usiku hatimaye wamesafirishwa kuja Dar es Salaam kwa  mabasi 9 yaliyokodiwa na Kampuni ya Reli Tanzania (TRL). Zoezi lilianza  saa  4:05  hadi saa 05:30 leo auibuhi.

Treni ya hiyo illikwama tokea usiku wa kuamkia leo kufuatia treni ya mizigo iliokuwa ikienda bara kupata ajali ya mabehewa yake mawili kuacha njia kati ya stesheni za Pugu na Pugu Mpiji.

Tayari wakati taarifa hii ikitolewa njia imefunguliwa kwa shughuli za uendeshaji wa reli ya kati kuendelea.



Imetolewa na Afisi ya Uhusiano:
 Kwa niaba ya  Mkurugenzi Mtendaji wa TRL
Ndugu Masanja Kungu Kadogosa
Novemba 28, 2016

DAR ES SALAAM
Treni ya abiria ya deluxe
 

No comments