Ads

UONGOZI WA TRL WAMEZINDUA HUDUMA MAALUM YA USAFIRISHAJI SHEHENA WA ‘BLOCK TRAIN KWENDA BURUNDI MACHI 31, 2017 KUTOKA MALINDI YARD BANDARINI.


(TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI (PRESS RELEASE)




Imefahamika kuwa  huduma maalum ya usafirishaji shehena wa treni nzima ‘block train’ imezinduliwa rasmi na Uongozi  wa TRL kwenda Burundi katika  kituo cha Malindi bandarini Dar es Salaam Machi 31, 2017.

Huduma ya block train iliozinduliwa ni maalum kwa wafanyabiashara na kampuni binafsi  wenye  shehena  kubwa za mizigo kutosheleza mabehewa 20 ambapo hurahisisha kuisafirisha moja kwa moja hadi kwa mpokeaji( mwenye mzigo).

Kwa mujibu wa taarifa ya Uongozi wa TRL treni hiyo yenye mabehewa 20 imebeba malighafi ya chuma( iron coils) mzigo unaosafirishwa na Kampuni ya UBUCOM ya Burundi na utachukua muda wa siku 3 kuwasili Kigoma na siku moja kuwasili mjini Bujumbura. Burundi.

Aidha taarifa zaidi zimeainisha kuwa TRL imepunguza gharama za usafirishaji wa mizigo ya kawaida (loose cargo) na ile iliohifadhiwa katika makasha kwenda Burundi. Hivi sasa TRL inatoza jumla ya Dola za Kimarekani (USD)3,056 kwa behewa moja la mizigo ya kawaida na USD 3024/= kwa mizigo iliofungwa katika makasha hadi Bujumbura Burundi ikilinganishwa na  gharama ya  USD 3500/= ikisafirishwa barabarani.
Gharama za TRL zinahusisha pia  uhudumiaji shehena bandarini  Dar es Salaam, Kigoma na Bujumbura na pia usafiri wa reli hadi Kigoma na wa meli hadi Bujumbura.


Imetolewa na Afisi ya Uhusiano kwa Niaba ya :
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TRL,
Nd Shaban Jumbe  Kiko,
Dar es Salaam,

Machi 31, 2017

No comments