Ads

MATUKIO MUHIMU YA TRL KATIKA PICHA 2016 ! - 1



UTEUZI WA MKURUGENZI MTENDAJI MPYA WA TRL 


Waziri wa Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mnyaa Mbarawa  Februari 2, 2016 alitangaza  uteuzi wa  Nd Masanja Kadogosa kuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) kuchukua nafasi ya Mhandisi Elias Mshana ambaye alikuwa anakaimu nafasi hiyo kuanza likizo ya kustaafu. Uteuzi huo ulianza mara moja.
Kabla ya Uteuzi huo Nd Kadogosa alikuwa Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB)



Nd. Masanja Kungu Kadogosa Mkurugenzi Mtendaji TRL



Aidha mnamo Julai 01, 2016,  Nd Kadogosa alithibitishwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji kamili wa TRL.


MARA TU BAADA YA UTEUZI ALIANZA KAMPENI DHIDI YA UBADHIRIFU NDANI NA NJE YA TRL  NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA



Nd. Masanja Kadogosa Mtendaji Mkuu wa TRL akifanya kampeni Buguruni kwa Mnyamani na Tabata Mwananchi dhidi ya wizi wa kokoto katika njia ya reli ya Dar hadi Ubungo Maziwa mwezi Juni, 2016


Nd. Masanja Kadogosa Mtendaji Mkuu wa TRL akizungumza na Wanareli mara baada ya zoezi la usafi ambalo hufanyika kila siku ya Jumamosi inayoangukia juma la mwisho la mwezi.
Nd. Masanja Kadogosa Mtendaji Mkuu wa TRL akizungumza na Wanareli mara baada ya zoezi la usafi ambalo hufanyika kila siku ya Jumamosi inayoangukia juma
la mwisho la mwezi.




































No comments