WALIOGAWA MAENEO YA HIFADHI YA RELI KUSHUGHULIKIWA NA SERIKALI!
WALIOGAWA MAENEO YA HIFADHI YA RELI KUSHUGHULIKIWA NA SERIKALI!
SERIKALI imesema inawafuatilia baadhi ya viongozi waliotumia madaraka yao vibaya kwa kuwapatia wananchi maeneo ya hifadhi za reli huku wakijua ni kinyume cha sheria.
Pia imetenga TZS.bilioni 14 kwa ajili ya kurudisha njia ya reli ya Arusha hadi Moshi kutokana na eneo hilo kuonekana kuwepo na wafanyabiashara wengi.
Tamko hilo lilitolewa na Naibu Waziri wa Uchukuzi kupitia Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye jijini Dar es Salaam jana, wakati alipofanya ziara ya kutembelea Kampuni ya Reli nchini (TRL) kwa lengo la kujitambulisha tokea baada ya kuteuliwa na Rais Dk. John Magufuli katika wadhifa wa Naibu Waziri katika Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano akisimamia sekta za Uchukuzi na Mawasiliano.
Pia imetenga TZS.bilioni 14 kwa ajili ya kurudisha njia ya reli ya Arusha hadi Moshi kutokana na eneo hilo kuonekana kuwepo na wafanyabiashara wengi.
Tamko hilo lilitolewa na Naibu Waziri wa Uchukuzi kupitia Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye jijini Dar es Salaam jana, wakati alipofanya ziara ya kutembelea Kampuni ya Reli nchini (TRL) kwa lengo la kujitambulisha tokea baada ya kuteuliwa na Rais Dk. John Magufuli katika wadhifa wa Naibu Waziri katika Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano akisimamia sekta za Uchukuzi na Mawasiliano.
Alisema viongozi hao ni lazima wafuatiliwe kwani wamekuwa sababu ya kuwepo kwa changamoto nyingi katika taasisi ya usafiri wa reli nchini.
Mhandisi Nditiye alisema changamoto hizo zimetokana na baadhi ya wajanya kushirikiana na wananchi kuweza kuvamia maeneo ya reli huku wakitambua kuwa ni kinyume cha sheria.
“Kwa wafanyakazi waliofanya hivyo ni lazima tuwafuatilie kwani lazima tujenge utamaduni kwa wananchi wa kuweza kuheshimu mali za serikali,” alisema.
Pia kutokana na hilo, Mhandisi Nditiye aliwataka wananchi wote waliojenga eneo lolote la hifadhi ya reli kubomoa mara moja ili kupisha mradi wa ujenzi na uboreshaji wa reli nchini.
Alifafanua kwa wananchi ambao mradi wa reli umegusa maeneo yao , Serikali imeiomba Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi kufanya tathimini kwa ajili ya kuwalipa.
Kwa upande mwingine, Mhandisi Nditiye, aliwaasa wafanyakazi wa TRL kuhakikisha wanafanya kazi kwa kusimamia mpango wa maendeleo na kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“ Haitapendeza kuona mtu anaenda kinyume na azma ya serikali katika utekelezaji wa majukumu kwani hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake,” alisema.
Kwa upande mwingine serikali imetenga TZS. bilioni 14 kwa ajili ya kurudisha njia ya reli ya Arusha hadi Moshi kutokana na eneo hilo kuwepo na wafanyabiashara wengi.
Akitolea ufafanuzi suala hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa TRL, Nd. Masanja Kadogosa alisema njia hiyo inatarajiwa kuwa tayari kutumika ifikapo Julai mwaka 2018 ambapo kiasi cha fedha kilichotengwa kitasaidia kukarabati madaraja na vituo vya reli.
“ Tunafanya hivyo kwa eneo Arusha hadi Moshi kwani limeonekana kuwa na biashara nyingi, hivyo tunawaomba wananchi wakae mkao wa kula ili kuwezesha serikali kupata mapato yanayostahili kupitia sekta ya usafiri wa reli,”alisema.
Hata hivyo alizitaja baadhi ya changamoto wanazokabiliwa nazo kuwa ni jinsi ya upatikanaji wa vibali vya wafanyakazi wa kigeni, Vitendea kazi na Ubovu wa mtandao wa reli ya kati ambao umechakaa kwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 100.
Naibu Waziri wa Uchukuzi kupitia Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye akizungumza na Waandishi wa Habari hapo jana. |
Pichani Waandishi wa habari wakiwa kazini. |
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawsiliano ( Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano) , Mhandisi Atashasta Nditiye hapo jana. akizungumza na Waandishi wa habari. |
Post a Comment