Ads

TRENI YA USIKU KWENDA PUGU KUANZA TENA LEO JANUARI 25, 2017!



KAMPUNI YA RELI TANZANIA(TRL)


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI (PRESS RELEASE)

SAFARI YA TATU AWAMU YA JIONI KWA TRENI YA PUGU KUANZATENA LEO 
JANUARI 25, 2017

Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) unayo furaha kuwatangazia umma wa Tanzania na Wasafiri wetu wa treni ya  mjini (commuter train) iendayo Pugu  kuwa safari ya tatu awamu ya jioni itaanza tena leo siku ya Jumatano Januari  25, 2017. Safari hiyo huanza Kituo kikuu  cha Dar es Salaam saa 2:15 usiku na kuwasili Pugu saa 3:10.

Kuanza tena kwa safari hiyo kunatokana na kukamilika kwa kazi ya kutandika reli mpya katika eneo korofi kati ya vituo vya  Ilala Block Post na Karakata.

Hata hivyo kwa awamu ya asubuhi safari zitaendelea kuwa mbili tu kwa vile kazi ya utandikaji reli bado haujakamilika .Kazi ya ukarabati wa njia ya reli kati ya vituo vya Dar es Salaam  na Pugu  ulianza  rasmi hapo Januari 02, 2017.

Kazi ya ukarabati huanza kati ya saa 3:15 (09:15 hrs) asubuhi hadi saa 8:15 (14:15 hrs) mchana  kila siku  za kazi  na inatarajiwa kukamilika baada ya majuma  ( wiki) 10 na tayari majuma ( wiki ) 4 yamekamilika tokea ianze kazi hiyo.

Ukarabati huu una lengo la kuimarisha njia ya reli katika eneo hii ambalo kwa sasa linapitisha treni nyingi sana kwa siku kuliko ilivyokuwa imezoeleka.

Aidha,  ukarabati huu utaondoa kero ya vumbi kwa abiria kwenye mabehewa   kwani njia yote itawekewa  kokoto za kutosha (stone ballast) ambazo hazina vumbi.


Ukarabati huu ni wa kubadilisha reli ndogo za ratili 60   na kuweka reli  kubwa za ratili 80 ambazo ni imara zaidi na kuwezesha  kutembea kwa usalama zaidi.

Imetolewa na Afisi ya  Uhusiano  kwa Niaba ya:
Mkurugenzi Mtendaji wa TRL,
Ndg. Masanja Kungu Kadogosa,
Dar es Salaam
Januari 25, 2017

No comments